Kiongozi wa muungano wa NASA Bwana Raila Odinga amesema kuwa muungano wake utafuata sheria za katiba kuwasilisha lalama zao za kuonyesha kuwa hawana imani na serikali ya Jubilee, Haya yanajiri baada ya Bwana Odinga kuapa kuwa ataapishwa mnamo Disemba 12. Aliyasema haya kwenye barabara ya Manyanja jijini Nairobi.
Odinga pamoja na wafuasi wake wameapa kutomtambua Rais Uhuru Kenyatta kuwa rais wa kenya wakisema kuwa hakuchaguliwa kwa njia halali
![]() |
| Picha ya Kinara wa NASA Raila Odinga |
Akizungumza na kituo cha CNN Odinga alisema kuwa yuko makini katika kudumisha katiba na utawala wa sheria hata baada ya kusema siku ambayo ataapishwa licha ya hatua hiyo kusemwa kuwa ni ukiukaji wa katiba. Odinga aliongeza kuwa yuko tayari kwa mazungumzo.
