Monday, 11 December 2017

MAHAKAMA KUTOA RIPOTI KUHUSU KUIDHINISHA USHINDI WA RAIS KENYATTA

Majaji wa mahakama ya juu siku ya leo (Jumatatu) wanatarajiwa kuelezea kikamilifu sababu zilizopelekea kuafikia uamuzi wa kuidhisha ushindi wa rais Uhuru Kenyatta kwenye uchaguzi wa Oktoba 26

Msajili wa mahakama alisema kuwa uamuzi utaanza kutolewa sa nane ikiongozwa na jaji mkuu David Maraga na naibu jaji mkuu Philomena Mwilu huku wakitarajiwa kuelezea ni kwa nini waliidhinisha ushindi wa rais Uhuru Kenyatta. Majaji wengine ambao watakuwepo ni Jaji Jackton Ojwang, Smokin Wanjala, Njoki Ndung'u na Isaac Lenaola

Image result for PHOTO OF PANEL OF JUDGES OF KENYA
Supreme Court Judges
Mahakama pia inatarajia kuelezea iwapo uchaguzi uliathirika ikizingatiwa kuwa maeneo bunge 25 hazikushiriki kwenye uchaguzi. Kesi mbili zilipelekwa mahakamani kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika marudio ya uchaguzi uliofanyika

Njonjo Mue na Khalef Khalifa walidai kuwa uchaguzi uliendashwa pasi na kufuata katiba na ilivyoagizwa na mahakama mnamo september 1. Mwanasiasa Harun Mwau naye alipeleka kesi mahakamani huku akidai kuwa tume ya IEBC iliendesha uchaguzi bila kufanya upya zoezi la uteuzi la majina ya wawaniaji urais kabla ya kuchapisha majina ya nane hao


No comments:

Post a Comment

WHAT DOES IT TAKE TO BE A LANDLORD IN TOWN?

 By Sifuma N. Lilian In light of the recent demolitions that are happening in the capital, it is always good to ensure that you’re follo...