Uchaguzi huu uliweza kukuja na maafa mengi takriban visa 86 vya ukatili wa kijinsia vikiripotiwa katika jiji la Nairobi wakati na hata baada ya uchaguzi.
Kulinganana ripoti ya shirika la kutetea haki za kibinadamu Kenya National Commission on Human rights (KNHCR) inasemekana asilimia 62 ya visa hivi viliendelezwa na maafisa wa polisi huku asilimia 38 ikiendelezwa na raia. Ripoti hiyo pia inaonyesha kuwa watu 35 waliuawa kati ya mwezi Septemba na Oktoba. Ripoti hii inajiri baada ya shirika hilo awali kutoa ripoti nyingine ilioonyesha visa 57 vya watu waliouawa wakati wa uchaguzi mkuu.
| Polisi wakiwakabili waandamanaji |
Kati ya waliouawa ni watoto, wanawake wawili na wengine wakiwa wanaume kati ya umri wa miaka 18 na 50. Mwenyekiti wa KNHCR Kagwiria Mbogori alisema kuwa wahasiriwa wote waliaga kutokana na risasi isipokuwa wawili
No comments:
Post a Comment