akiwahutubia huko mombasa katibu katika wizara ya elimu Dkt.Richard Belio Kipsang' alisema kuwa serikali imeweka mikakati ambayo itahakikisha elimu bila malipo kwa shule za upili inafanikishwa.
| Kongamano la walimu mjini Mombasa |
Hata hivyo swala la kuwa na mwalimu mkuu mmoja wa shule za msingi na upili zinazotumia ua moja liliweza kupingwa na baadhi ya wakuu hao huku wakitaja hatua hiyo kama itakayochangia kusambaratika kwa viwango vya elimu hapa nchini na hivyo kupendekeza kuwepo kwa mikakati maalum itakayowezesha ufanisi wa elimu bila malipo kwa shule za upili
Vilevile mpango wa usambazaji vitabu katika shule za msingi na upili zinatarajiwa kuanza mapema hapo mwakani huku takriban wanafunzi millioni tisa wakitarajiwa kunufaika na mpango huu. Wachapishaji wa vitabu humu nchini pia hawajakumbatia mabadiliko haya huku wakiwa na hofu ya kutochaguliwa kwa mashirika yao huku ya kiserekali yakipewa kipao mbele.
No comments:
Post a Comment