Waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang'i amewapa wafanyi biashara kutoka nchi za kigeni siku 60 kupata kibali halali cha kuendesha biashara la sivyo wafurushwe kutoka nchini.
Kwa mujibu wa rekodi za serikali vibali elfu 34,000 vimepeanwa kufikia sasa ilhali kuna zaidi ya wafanyibiashara laki moja nchini utoka nchi za kigeni .Aidha Dkt. Matiang'i aliongeza kwamba kukosa kwa wafanyibiashara hao vibali kunahujumu usalama wa taifa na kuinyima nchi kipato.


