Mvua inayoendelea kunyesha nchini imekuwa karaha na si furaha tena kwa wakaazi maeneo mbalimbali nchini.
Nyingi za shule zimelazimika kufungwa sababu kuu zikitokana na mvua ambayo imesababisha vyoo shuleni kuzama,hali ambayo hairuhusu masomo kuendelea kama kawaida.
Idara ya afya hii leo imefunga shule ya msingi ya Kapsaret kwenye kaunti ya Uasin Gishu kwa muda usiojulikana baada ya kuzama kwa vyoo shuleni humo kufuatia mvua kubwa inayoendelea kunyesha eneo hilo.

No comments:
Post a Comment